TRUMP AWAITA ' VIBAKA ' WAANDAMANAJI WANAOPINGA MAUAJI YA MMAREKANI MWEUSI YALIYOFANYWA NA POLISI


Rais Donald Trump wa Marekani  amewaita waandamanaji wanaopinga mauaji ya Mmarekani mweusi George Floyd katika mji wa Minneapolis kuwa ni "vibaka" na kuonya kwamba watafyatuliwa risasi iwapo wataanza kupora.
 


Trump aliandika kwenye ukurasa wake wa twitter baada ya waandamanaji hao walioghadhabishwa na kifo cha Floyd chini ya mikono ya polisi, kuchoma kituo cha polisi. 

Mapema, Trump alielezea kusikitishwa na kifo hicho akisema lilikuwa ni tukio la kushtusha mno. 

Hata hivyo, alibadilika baada ya machafuko hayo ya jana usiku na kusema kuwa vibaka hao wanachafua kumbukumbu ya Floyd na hatakubali hali hiyo kutokea.

 Alisema amezungumza na gavana Tim Walz na kumueleza kwamba jeshi liko upande wake, na iwapo wataanza uporaji wafyatuliwe risasi.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527