SHERIA YA KODI YATOA MSAMAHA KWA MAPATO YASIYOZIDI MILIONI 4 KWA MWAKA

Na. Josephine Majura na Saidina Msangi, WFM, Dodoma

Serikali imeeleza kuwa Sheria ya Kodi imetoa msamaha wa kodi kwa wafanyabiashara ikiwa ni pamoja na wastaafu ambao mapato yao kwa mwaka hayazidi Shilingi milioni nne.

Hayo yameelezwa jijini Dodoma na Naibu Waziri wa Fedha na Mipango, Dkt. Ashatu Kijaji, alipokuwa akijibu swali la msingi la Mbunge wa Lupembe, Mhe. Joram Ismael Hongoli, aliyetaka kujua sababu za Serikali kutoweka utaratibu wa kutowatoza kodi wastaafu ambao biashara zao hazizidi mtaji wa Shilingi milioni nne.

Dkt. Kijaji alisema kuwa wastaafu walioanzisha miradi midogo ya kilimo na biashara ambayo inawaingizia kipato kisichozidi Shilingi milioni nne hawapaswi kutozwa kodi kwa kuwa Sheria ya Kodi imetoa msamaha.

Alisema kuwa Kifungu cha nne cha Sheria ya Kodi ya Mapato kinatoa msamaha wa kodi ya mapato kwa mfanyabiashara ambaye mapato yake ghafi ya mwaka hayazidi Sh. milioni 4, hii ikiwa ni pamoja na mapato ya wafanyabiashara wastaafu ambao kiwango chao cha mapato hakizidi kiasi hicho kwa mwaka.

Mwisho.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527