RAIS MAGUFULI AONGOZA KIKAO CHA BARAZA LA MAWAZIRI IKULU DODOMA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt. John Pombe Magufuli ameongoza Kikao cha Baraza la Mawaziri kilichofanyika katika Ukumbi wa Baraza la Mawaziri Ikulu ya Chamwino mkoani Dodoma.


Kikao hicho kimehudhuriwa pia na Makamu wa Rais Mhe. Samia Suluhu Hassan, Waziri Mkuu Mhe. Kassim Majaliwa, Mawaziri pamoja na Manaibu Mawaziri tarehe 27 Mei 2020.

Awali kabla ya kikao hicho Mhesimiwa Rais aliwaongoza wajumbe kusimama kwa dakika moja ili kumkumbuka na kumuombea aliyekuwa Waziri wa Katiba na Sheria Marehemu Balozi Dkt. Augustine Mahiga kabla ya kuanza kwa Kikao hicho.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527