IRAN YAWAUA WANAJESHI WAKE KIMAKOSA KATIKA JARIBIO LA KOMBORA JIPYA


Wanamaji 19 wameuawa na wengine 15 wakajeruhiwa katika tukio la ajali lililohusisha meli za kijeshi za Iran katika Ghuba ya Oman , jeshi la Iran limesema.

Vyombo vya habari vya Iran vimesema kwamba meli hiyo kwa jina Konarak ilishambuliwa na kombora jipya lililokuwa likijaribiwa na meli ya kijeshi ya Frigate Jamaran wakati wa zoezi la kijeshi siku ya Jumapili.

The Konarak ilishambuliwa na kombpora jipya Jumapili mchana wakati wa zoezi la kijeshi katika maji ya Bandar-e Jask kusini mwa pwani kulingana na runinga ya taifa katika tovuti yake.

Wanamaji hao walisema kwamba meli hiyo ilivutwa hadi ufukweni na kwamba uchunguzi umeanza.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527