Tanzia: JAJI MKUU MSTAAFU, AUGUSTINO RAMADHANI AFARIKI DUNIA


Jaji Mkuu Mstaafu wa Tanzania, Augustino Ramadhani amefariki dunia leo asubuhi katika Hospitali ya Aga Khan, jijini Dar baada ya kuugua maradhi ya moyo.


Familia yake imesema hali ya Jaji Ramadhani ilibadilika jana usiku na kukimbizwa hospitalini hapo ambapo mauti ilimkuta leo asubuhi.


Jaji Augustino Ramadhani pia alikuwa Brigedia Jenerali kabla ya kuitwa katika sekta ya Sheria na kutumikia Mahakama.

Alipostaafu ujaji, alipewa kazi ya ukasisi, akatawazwa rasmi kuwa Mchungaji wa Dayosisi ya Kanisa la Anglikana lililopo Mkunazini Zanzibar na hivyo kuitwa “Mchungaji Augustino Ramadhani”


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post