PROFESA ANNA TIBAIJUKA AAGA BUNGE KWAMBA HATAGOMBEA TENA


Mbunge wa Muleba Kusini Balozi Profesa Anna Tibaijuka, leo Aprili 3, 2020, amewaaga rasmi Wabunge wenzake na kusema Bunge lijalo atakua ameng'atuka madarakani na kwamba anaenda kuandika kitabu chake.



Aidha Profesa Tibaijuka akizungumzia suala la Virusi vya Corona, ameiomba Serikali kuangalia njia mbadala ikiwemo kutumia tiba za asili ili kuweza kukabiliana na ugonjwa huo kwa sababu hao wazungu wanaotuletea tiba zao sasa, hapo kabla walitukuta na tiba zetu za asili.

"Sisi lazima tuwe na mpango mbadala ambao unajikita kwenye jamii yetu, inabidi tuseme tiba zetu mbadala ziko wapi, hakuna jamii itakayokaa kusubiri kifo lazima itajihami, tayari nimemuandikia barua Dkt Ndugulile ya kwamba lazima tuangalie Plan B, nashukuru sana wananchi wa Muleba kwa kunipa nafasi kwa miaka 10 nimejifunza mengi, naenda kuandika kitabu" amesema Profesa Tibaijuka.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527