MILTON LUPA NFRA KUANZA KUNUNUA MAHINDI, MTAMA NA MPUNGA


Serikali kupitia Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) imeanza kujipanga kuanza kununua mazao ya nafaka kwa wakulima ili punde tu mazao yatakapovunwa shambani yaweze kununuliwa na kuhifadhiwa kwa ajili ya akiba ya chakula.


Afisa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Taifa wa Hifadhi ya Chakula (NFRA) Ndg Milton Milos Lupa amemuhakikishia katibu Mkuu wa Wizara ya Kilimo ya Kilimo Ndg Jerald Kusaya wakati wa ziara yake ya kikazi ya siku moja NFRA Makao makuu Jijini Dodoma kuwa tayari wataalamu wapo mikoani kwa ajili ya kazi hiyo.

Lupa amesema kuwa msimu wa kilimo wa mwaka 2019/2020 NFRA itanunua mazao makuu matatu ambayo ni zao kuu la chakula Mahindi, Mpunga na Mtama.

Amesema kuwa lengo la serikali kuamua kununua mazao hayo matatu ni kujiimarisha vyema katika uhifadhi wa chakula ili inapotokea dharula ya chakula nchini kuwe na hifadhi ya mazao tofauti tofauti.

Akizungumzia lengo la Wakala kuanza kujipanga ili kununua nafaka mapema, amesema kuwa lengo la kufanya hivyo ni kupata mazao bora kwa ajili ya kuhifadhi kadhalika kupata mazao mengi.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post