RC MBEYA ATOA AMRI BAA ZOTE ZIFUNGWE SAA TATU USIKU ILI KUKABILIANA NA CORONA


Mkuu wa Mkoa wa Mbeya Albert Chalamila ametoa amri kwa wamiliki wa maeneo yote yanayouzwa pombe (Bar) kufunga biashara zao kila ifikapo saa tatu kamili usiku kuanzia jumatatu  kwa lengo la kuepusha misongamano inayoweza kusababisha watu kuambukizana corona. 


Ametoa agizo hilo jana April 17, 2020 baada ya kutembelea bar kadhaa na kukuta watu wakiwa kwenye misongamono iliyopigwa marufuku


"Walevi wanaoanza kunywa pombe kuanzia saa tatu kwenda mbele huwa hawana utambuzi wa kuachiana nafasi na kwa mantiki hiyo hupiga story na kushikashikana" -Alisema


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527