MKUU WA JESHI LA ZIMAMOTO NA UOKOAJI AFANYA MABADILIKO YA MAKAMANDA


Mkuu wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji, (CGF) John W. Masunga, amefanya mabadiliko ya baadhi ya Makamanda wa Mikoa.

Makamanda walioguswa na mabadiliko hayo ni Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Zimamoto na Uokoaji (SACF) ABDALLAH MAUNDU anakwenda kuwa (RFO) Kamanda wa Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Kigoma, kabla ya nafasi hii
alikuwa Makao Makuu Dodoma.

Aliyekuwa Kamanda wa Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Mara, Kamishna Msaidizi Mwandamizi (SACF) SALUM M. OMARI, anayekwenda kuwa (RFO) Kamanda wa Mkoa wa Kinondoni, kuchukua nafasi ya Mrakibu Msaidizi wa
Zimamoto na Uokoaji (ASF) JENIFER V. SHIRIMA anayehamia Makao Makuu kuwa Mkuu wa dawati la Mambo ya Nje.

Aidha nafasi ya (RFO) Kamanda wa Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Mara inachukuliwa na Mrakibu Msaidizi wa Zimamoto na Uokoaji (ASF) AUGUSTINE B. MAGERE.

Pia aliyekuwa Kamanda wa Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Temeke, Kamishna Msaidizi Mwandamizi (SACF) ELIA P. KAKWEMBE, anayekwenda kuwa (CFO) Kamanda wa Viwanja vya Ndege Nchini, kuchukua nafasi ya Kamishna Msaidizi (ACF) BAKARI K. MRISHO anayekwenda kuwa (RFO) Kamanda wa Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Temeke.

Aliyekuwa Kamanda wa Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Shinyanga Mrakibu wa Zimamoto na Uokoaji (SF) OMARI H. SIMBA anayekwenda kuwa (RFO) Kamanda wa Mkoa wa Simiyu na nafasi yake inachukuliwa na Mrakibu wa
Zimamoto na Uokoaji (SF) GEORGE G. MRUTU anayetoka Makao Makuu.

Mabadiliko haya ni ya kawaida kwa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527