Picha : MWILI WA MTANGAZAJI WA TBC MARIN HASSAN MARIN WAZIKWA ZANZIBAR

WANANCHI wakibeba Jeneza lililokuwa na Mwili wa Marehemu Marin Hassan Marin, wakitoka nyumbani kwa marehemu na kuelekea katika Msikiti wa Kibweni KMKM kwa ajili ya kuombea dua kwa ajili ya maziko yaliofanyika katika makaburi ya Mwanakwerekwe Jijini Zanzibar leo Aprili 2,2020.(Picha na Othman Maulid )
WAUMINI wa Dini ya Kiislam wakiuombea dua mwili wa Mwandishi wa Habari Mwandamizi wa Shirika la Habari Tanzania (TBC) baada ya kumalizika Sala ya Maiti iliofanyika katika Msikiti wa KMKM Kibweni Jijini Zanzibar.(Picha na Ikulu)
WAZIRI wa Habaro Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar.Mhe. Mahmoud Thabot Kombo akizungumza na kutowa shukrani kwa niaba ya Wizara yake wakati wa hafla ya maziko ya Mwandishi wa Habari Muandamizi Tanzania Marehemu Marin Hassan Marin, yaliofanyika katika makaburi ya Mwanakwerekwe Jijini Zanzibar.(Picha na Othman Maulid)
MAWAZIRI wa Habari wa SMT na SMZ. Kushoto Waziri Habari Utalii na Mambo ya Kale Zanzibar Mhe. Mahmoud Thabit Kombo na Waziri wa Habari Utamaduni Sanaa na Michezo Mhe. Dkt. Harrison Mwakyembe, wakiwasili katika viwanja vya Msikiti wa Kibweni KMKM kuhudhuria maziko ya Mwandishi wa Habari Mwandamizi wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) Marin Hassan Marin, yaliofanyika leo 2/4/2020 na kuzikwa katika makaburi ya Mwanakwerekwe Wilaya ya Magharibi “B” Unguja.(Picha na Othman Maulid)
WANAICHI na Waumini wa Kiislam wakiitikia dua baada ya kumalizika kwa maziko ya Marehemu Marin Hassan Marin Mwandishi wa Habari Muandamizi wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC) yaliofanytika katika makaburi ya Mwanakwerekwe Wilaya ya Magharibi “B” Unguja leo 2/4/2020.(Picha na Othman Maulid)

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post