MAKONDA: KUANZIA JUMATATU KILA MTU LAZIMA AVAE MASK NA BIASHARA ZOTE ZIFANYIKE KWA 'TAKE AWAY'


Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda leo Aprili 18, 2020 amesema, kuanzia Jumatatu, Aprili 20, 2020 kila anayekwenda sehemu ya manunuzi, lazima avae barakora na kuwataka wafanyabiashara kufanya biashara  zote kwa njia ya 'take away'.
“Anayekwenda eneo la manunuzi yotote lazima awe amevaa barakoa (mask), ununue,ukate leso, ukate kanga utaamua wewe, lakini lazima uwe umevaa


"Pia kuanzia Jumatatu biashara zote zifanyike katika mfumo wa ‘take away’ ukienda sehemu nunua ondoka, lazima pia kuwe na hatua mita mbili katika msongamano wa Watu”- Amesema RC Paul Makonda 

Amewataka wenye masoko kutumia njia mbadala wa kufanya kazi kwenye masoko yao ili kujikinga na corona


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527