WAGONJWA WA CORONA TANZANIA WAFIKA 88...WAMEONGEZEKA 29...HADI LEO WALIOPONA 11, VIFO VINNE



Wizara ya Afya,Maendeleo ya Jamii,Jinsia,Wazee na Watoto Nchini Tanzania imetoa taarifa ya uwepo wa Wagonjwa 29 waliothibitika kuwa na Ugonjwa wa Corona nchini Tanzania ambapo kati yao 26 wapo Dar es salaam, Wawili Mwanza na mmoja yupo Kilimanjaro na wote wanaendelea na matibabu chini ya uangalizi wa wataalamu wa afya.

Aidha taarifa hiyo inasema wagonjwa waliopona hadi leo Aprili 15,2020 ni 11,vifo vitokanavyo na Covid 19 ni vinne


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post