WAHUDUMU WA HOTELI WAAMBUKIZWA CORONA


Idadi ya visa vya waathirika wa Virusi vya Corona nchini Kenya imeongezeka na kufikia visa 246, baada ya hii leo kutangaza visa vipya 12, huku watano kati yao ni wakiwa ni wafanyakazi wa hoteli.

Taarifa hiyo imetolewa leo Aprili 17, 2020 na Waziri wa Afya wa Kenya Mutahi Kagwe, na kusema kuwa kwa kipindi cha masaa 24, nchi hiyo tayari imekwishapima sampuli za watu 450.

"Mpaka asubuhi hii ninavyoongea tayari ndani ya masaa 24 tumekwishapima sampuli 450 na kati ya hao tuliowapima tumepata wagonjwa 12, na siku yenyewe bado haijaisha na watano kati yao ni wafanyakazi wa hoteli" amesema Waziri wa Afya Mutahi Kagwe.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post