UTURUKI YAWAUWA WANAJESHI 19 WA SERIKALI YA SYRIA


Mashambulizi ya angani ya ndege za Uturuki zisizoruka na rubani yamewauwa wanajeshi 19 wa serikali ya Syria katika mkoa wa kaskazini magharibi wa Idlib, wakati mvutano ukiendelea kati ya Syria na Uturuki. 

Shirika linalofuatilia haki za binaadamu nchini Syria limesema wanajeshi hao waliuawa baada ya msafara wao kushambuliwa katika eneo la Jabal al-Zawiya na kituo cha kijeshi karibu na mji wa Maaret al-Numan. 

Ripoti hiyo imekuja saa chache baada ya Uturuki kuzidungua ndege mbili za kivita za Syria, katika operesheni kali inayofanywa dhidi ya serikali ya Syria mkoani Idlib, ambako wanajeshi waasi wakisaidiwa na Uturuki wanaweka kizingiti kwa serikali ya Damascus kuchukua udhibiti wa nchi nzima. 

Uturuki imethibitisha kuanzisha operesheni kamili dhidi ya wanajeshi wa Syria wanaoungwa mkono na Urusi baada ya wanajeshi 34 wa Uturuki kuuawa wiki iliyopita katika shambulizi la angani lililodaiwa kufanywa na serikali ya Syria.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527