Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) Yampongeza Rais Magufuli Kwa Kukutana na Wapinzani

Tume ya Haki za Binadamu na Utawala Bora (THBUB) imemuomba Rais wa Tanzania, John Magufuli kuendeleza utaratibu wa kukutana na viongozi wa vyama vya upinzani na makundi mengine kila atakapopata nafasi.

Kauli hiyo imekuja ikiwa ni siku chache tangu, Rais Magufuli kukutana na viongozi wa vyama vitatu vya upinzani na kufanya nao mazungumzo Ikulu, Dar es Salaam.

Tume hiyo imeeleza hayo leo Ijumaa Machi 6, 2020 katika tpitia taarifa yao kwa vyombo vya habari iliyotolewa na kusainiwa na mwenyekiti wa tume hiyo, Jaji Mstaafu Mathew Mwaimu.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post