TFF, BODI YA LIGI KUU KUKUTANA KESHO KUANGALIA MUSTAKABALI WA LIGI KUTOKANA NA MLIPUKO WA VIRUSI VYA CORONA

Rais wa Shirikisho la soka nchini TFF, Wallace Karia ameeleza Kamati ya Uongozi ya Bodi ya Ligi kuu kuitisha kikao cha dharura kesho siku ya Jumatano ya Machi 18, 2020.



Kikao hicho kitakachoanza saa 3:00 asubuhi, kitafanyika katika Ukumbi wa Hoteli ya Golden Tulip, City Center Dar es Salaam.

Ajenda kubwa katika kikao hicho ni kuangalia mustakabali wa ligi kutokana na mlipuko wa Virusi vya ugonjwa wa Corona ambao umeingia nchini.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527