MWALIMU AUAWA KWA KUPIGWA TOFALI BAADA YA KUGOMA KUNUNUA POMBE

Mwalimu wa Shule ya Msingi Mbugani kata ya Kakese mkoani Katavi Shauri Kiani (35) amefariki dunia baada ya kupigwa na tofali kichwani baada ya kukataa kumnunulia pombe anayetuhumiwa kuhusika na tukio hilo.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Katavi, Benjamin Kuzaga amesema tukio hilo limetokea Machi 3, 2020 saa 5 usiku eneo la Mbugani. 

Mtuhumiwa ni Omary Juma (30) mkazi wa Kakese. Kiani alikimbizwa hospitali ya rufaa ya mkoa wa Katavi lakini alifariki wakati anapatiwa matibabu.”

Amesema polisi walifika eneo la tukio na kumkamata mtuhumiwa anayeendelea kuhojiwa, kwamba muda wowote atafikishwa mahakamani.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post