MKUTANO WA KILELE WA G7 WAFUTWA KWA SABABU YA CORONA


Serikali ya Marekani imefuta mkutano wa ana kwa ana wa kilele wa wakuu wa kundi la mataifa yaliostawi zaidi kiviwanda duniani G7 uliokuwa umepangwa kufanyika mwezi Juni kutokana na janga la mripuko wa virusi vya corona. 


Badala yake viongozi hao wa serikali na mataifa saba watazungumza kwa njia ya video. 

Viongozi wa ngazi ya juu wa mataifa yaliostawi zaidi kiviwanda duniani ya Uingereza, Canada, Ufaransa, Ujerumani, Italia, Japan na Marekani, hukutana mara moja kwa mwaka kujadili masuala muhimu ya kidunia. 

Mwaka huu rais wa Marekani Donald Trump ndiye alipaswa kuwa mwenyeji wa mkutano huo.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527