MBUNGE WA MOSHI VIJIJINI, ANTONY KOMU ATANGAZA KUJIONDOA CHADEMA


Mbunge wa Moshi Vijijini, Antony Komu leo Machi 29, 2020 ametangaza kujiondoa kwenye Chama cha Demokrasia na Maendeleo mara baada ya kipindi chake cha ubunge kuisha na kusema atahamia chama cha NCCR Mageuzi.

Akizungumza na waandishi wa Habari katika Hotel ya Nepherland Magomeni Jijini Dar es salaam, Komu amedai kuwa anaamini Chama cha Demokrasia na Maendeleo ( CHADEMA) kitatumia busara kumuacha amalizie majukumu yake ya kibunge kwa muda uliobakia kwani bado anahitaji kuwatumikia wananchi wake.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527