KATIBU MKUU CCM: TUSIFURAHIE BENARD MEMBE KUFUKUZWA


Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi CCM Dkt Bashiru Ally, amemuomba aliyewahi kuwa Waziri wa Mambo ya Nje Bernard Membe, aache kutapatapa na kwamba anahitaji kufanyiwa ushauri wa kisaikolojia ili aweze kuwa sawa.


Dr Bashiru Ameyasema hayo wakati akizungumza  katika mahojiano yake na Gazeti la Mwananchi leo tarehe 2 Machi 2020 jijini Dar es Salaam

Amesema CCM wamechukua hatua hiyo baada ya hatua za awali kushindwa kufanikiwa....

"Ndugu Membe alishawahi kupewa adhabu ya onyo kali ikiwa ni hatua ya kujaribu kumpa nafasi ya kujirekebisha, lakini ilishindikana,  huu ni uamuzi mgumu tuliochukua, na si kusherehekea na nisingependa WanaCCM kujitokeza hadharani kufurahia.


" Nadhani tumpe muda, ni binadamu ana haki zake,  anahitaji ushauri nasaha, maana siyo tatizo dogo hili na mimi sitaki kulizungumza kwa ushabiki hata lingenipata mimi ningehitaji marafiki zangu wa karibu niwashirikishe" amesema Dkt Bashiru.
 
Dk. Bashiru ameeleza kuwa, milango ya CCM  kupokea wanachama wanaokiri makosa yao na kuomba msamaha iko wazi, hivyo Membe anaweza kukata rufaa juu ya suala hilo.

“Mchakato huu ni kama wa kimahakama kuna rufaa, nikianza mimi kusema wakati mimi ndio nitapokea rufaa kama nipo ni kama naingilia mchakato wa haki. Na matarajio yangu ni kwamba atarudi CCM, nikiwa hai au nimekufa.

“Sababu milango ya kuwapokea wanachama iko wazi na kuondoka iko wazi, mimi nimesaini barua za misamaha 14 na niko tayari kusaini ya 15 ambayo ni ya Membe kurudi kama akitaka,” amesema Dk. Bashiru.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post