CHADEMA WALIPA MILIONI 110 KUWATOA HALIMA MDEE, ESTER MATIKO NA ESTER BULAYA GEREZANI


Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimesema kimeanza mchakato wa kuwatoa gerezani mbunge wa Kawe, Halima Mdee; Esther Matiko (Tarime Mjini) na Ester Bulaya (Bunda).

Mkurugenzi wa itikadi, uenezi, mawasiliano na mambo ya nje wa Chadema, John Mrema amesema mpaka sasa wameshalipa faini ya Sh110 milioni iliyotakiwa kulipwa na wabunge hao watatu ili watoke gerezani.

Viongozi wanane wa Chadema pamoja na aliyekuwa Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Vicent Mashinji jana Jumanne Machi 10, 2020 walihukumiwa kulipa faini ya Sh350 milioni au kwenda jela miezi mitano baada ya kutiwa hatiani kwa makosa 12 kati ya 13 yaliyokuwa yanawakabili.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527