Burkina Faso yaripoti kifo cha kwanza cha Corona

Burkina Faso imetangaza kifo cha kwanza cha mtu aliyekuwa na ugonjwa wa Corona nchini humo, hii ikiwa ni kesi ya kwanza ya kifo kilichotokana na ugonjwa huo kuripotiwa katika eneo la chini ya jangwa la Sahara barani Afrika.

Profesa Martial Ouedraogo, mkuu wa jopokazi la kupambana na virusi vya Corona nchini humo amewaambia waandishi wa habari kuwa, aliyeaga dunia kwa Corona ni mwanamke wa miaka 62, aliyekuwa amelazwa katika chumba cha wagonjwa mahututi. 

Amesema mwanamke huyo ambaye pia alikuwa anaugua ugonjwa wa kisukari, aliaga dunia usiku wa kuamkia jana Jumatano.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post