URUSI NA UKRAINE ZARUSHIANA MAKOMBORA


Ukraine imesema mwanajeshi wake mmoja ameuawa na wengine kadhaa wamepata majeraha, katika makabaliano na vikosi vya Urusi ambavyo Ukraine imesema viliingia kwenye ardhi yake.

Tangazo la wizara ya ulinzi limesema kuwa mapigano hayo yalitokea katika mikoa minne ya mashariki mwa Ukraine ambayo ina wakaazi wachache.

Wizara hiyo imesema imeweza kujibu mapigo ya iliyemtaja kuwa adui yake, na kuweza kudhibiti hali ya mambo katika mkoa wa Luhansk.

Aidha, kulingana na tangazo hilo, mwanajeshi mmoja wa upande wa wanamgambo wanaoungwa mkono na Urusi ameuawa pia.

Kila upande unaushutumu mwingine kuvunja makubaliano yaliyosainiwa, yakihimiza kuondolewa kwa silaha nzito nzito.

Wiki iliyopita, Rais wa Ukraine Volodymyr Zelenskiy alifanya mazungumzo na mwenzake wa Urusi Vladimir Putin kwa njia ya simu, ambapo walikumbushana makubaliano mapya ya amani yaliyotiwa saini mjini Paris miezi miwili iliyopita.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527