ISRAEL YADAI KUISHAMBULIA SYRIA KWA MAKOMBORA


Israel inadai kuwa imevishambulia vituo vya kijeshi vya kundi lijiitalo Islamic Jihad karibu na mji mkuu wa Syria, Damascus. 

Taarifa ya jeshi la Israel inasema kuwa ndege zake zilipiga maeneo ya kundi hilo kusini mwa Damascus, kufuatia makombora yaliyorushwa kutoka Ukanda wa Gaza. 

Taarifa hiyo imesema pia kuwa jeshi la Israel lilirusha makombora yake kuelekea Gaza. 

Hata hivyo, shirika la habari la Syria, SANA, limesema kuwa mfumo wa ulinzi wa nchi hiyo ulifanikiwa kuyatunguwa makombora hayo. 

Kundi la Islamic Jihad linaendesha shughuli zake ndani ya Mamlaka ya Palestina na pia nchini Syria, na jana Jumapili lilirusha makombora yapatayo 20 kutokea Ukanda wa Gaza. 

Mashambulizi haya ya Israel yalifanyika muda mchache, baada ya jeshi kumuua kijana mmoja wa Kipalestina liliyedai alikuwa akitega bomu kwenye mpaka, na kisha kuiburuza maiti yake kwa buldoza, hali iliyozusha hasira kubwa kote Palestina.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post