IDADI YA VIFO KUTOKANA NA VIRUSI VYA CORONA YAFIKA 304 CHINA


Idadi ya vifo kutokana na janga la virusi vya corona nchini China imefikia watu 304 kufikia jana usiku, baada ya watu 45 kufariki dunia katika siku iliyotangulia. 

Tume ya Afya nchini humo imesema vifo hivi vipya vilitokea katika mkoa wa Hubei, ambao ndio kitovu cha mlipuko wa virusi hivyo. 

Kote nchini China, kulikuwa na maambukizi mapya ya watu 2,590 jana Jumamosi na kufikisha 14,380 jumla ya idadi ya watu walioambukizwa mpaka sasa. 

China inaendelea kutengwa wakati hatua za kudhibiti usafiri duniani zikiendelea kuchukuliwa na kufutwa safari za ndege. 

Janga hilo limesababisha mataifa mengi kuwahamisha raia wao huku mashirika ya ndege yakisitisha safari kwenda nchini humo. 

Hatua hiyo pia inatishia kuathiri kwa kiasi kikubwa kushuka uchumi wa taifa hilo la pili kwa ukubwa kiuchumi duniani. 

Kumeripotiwa zaidi ya visa 130 vya maambukizi ya virusi vya corona katika karibu nchi nyingine 24 duniani.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post