OMAR AL BASHIR KUPELEKWA MAHAKAMA YA ICC

Baraza la mpito Nchini Sudani limekubali kumkabidhi rais wa zamani Omar al Bashir kwa mahakama ya kimataifa ya ICC.


Omar al Bashir alikuwa akitafutwa kutokana na makosa ya uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya binaadamu.

Mwezi Desemba kiongozi huyo wa zamani aliyeondolewa madarakani kwa mapinduzi mwezi Aprili, alihukumiwa kifungo cha miaka miwili kwa makosa ya rushwa.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527