BASHE:HAKUNA MAENEO YALIYOSHAMBULIWA NA NZIGE NCHINI

Na Faustine Gimu
Naibu waziri wa kilimo MHE.HUSSEN BASHE amesema kuwa hakuna eneo lolote ambalo limeshambuliwa na nzige hapa nchini kutokana na taarifa ambazo zimekuwa zikizagaa mitandaoni.


MHE.BASHE amesema hayo mkoani Dodoma katika kongamano la wachambuzi  wa sera za kilimo nchini ambapo wadau hao wamekutana na kujadili mwenendo wa hali ya kilimo nchini.

Akizungumza katika kongamano hilo MHE.BASHE amesema kuwa serikali imejiandaa kwa ajili ya kupambana na janga hilo kwa kupeleka wataalamu maeneo mbalimbali pamoja na kuandaa dawa ili kupambana na tatizo hilo.

Katika hatua nyingine MHE.BASHE amesema kuwa kumekuwa na changamoto kwa watafiti na wachambuzi wa udongo ambao unafaa kutumia mbolea ambayo hali ambayo imeipelekea changamoto wizara hiyo jinsi ya kumfanya mkulima aweze kumudu gharama ya sampuli ambazo anatakiwa kutumia.

Kwa upande wake mkurugenzi mtendaji wa jukwaa huru la kilimo nchini ANSAF AUDAX RUKONGE ameeleza kuhusu soko la kahawa hapa nchini na kuwashauri wawekezaji kuwekeza zaidi kwa kufungua makampuni mengi.

Nao baadhi ya washirikio wameomba masuala mbalimbali yajashughulikiwe ili  kukuza sekta ya kilimo na ufugaji

Pia Wadau wa sekta ya kilimo wamejadili changamoto zanazoikabili sekta hiyo pamoja na kupatiwa ufumbuzi kupitia kongamano la sita la sera za kilimo ambapo linahitimishwa leo Februari 14,2020.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527