TMDA YAFANYA UKAGUZI VIWANDA VYA DAWA VINAVYOJENGWA DAR ES SALAAM NA PWANI


Kaimu mkurugenzi mkuu wa TMDA, Adam Fimbo (wa tatu kushoto) akipatiwa maelezo na watalaam wa ukaguzi wa viwanda katika moja ya kiwanda kinachojengwa.
Kaimu mkurugenzi mkuu wa TMDA, Adam Fimbo (katikati) akiwa katika picha ya pamoja kwenye moja ya viwanda walivyotembelea katika ukaguzi.
***
MAMLAKA ya Dawa na Vifaa tiba (TMDA), imefanya ziara ya kutembelea na ukaguzi wa viwanda 8 vya dawa za binadamu na mifugo vinavyoendelea kujengwa katika mikoa ya Pwani na Dar es Salaam.

Katika ziara hiyo, Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa TMDA, Adam Fimbo aliambatana na wakaguzi wa viwanda kuangalia hatua zilizofikiwa katika ujenzi na kuendelea kutoa ushauri wa kitaalam ili kuwezesha viwanda hivyo kukidhi matakwa ya kisheria katika utengenezaji sahihi wa dawa (GMP). 

Ziara hiyo ya siku tatu iliyoanza Januari 27-29 mwaka huu, ni katika kuunga mkono jitihada za Serikali ya Awamu ya Tano.

Viwanda vilivyotembelewa ni:- 

Vista Pharmaceuticals Ltd na Kariuki Pharmaceuticals vilivyopo Zegereni, Kibaha, Hester Biosciences Africa Ltd na Biotec Pharmaceuticals vya mifugo vilivyopo Kibaha, Emedics Pharmaceuticals kilichopo Kerege Bagamoyo.

Pia Cure Pharmaceuticals Ltd kilichopo Kimbiji, Kigamboni, African Pharmaceuticals kilichopo Kisemvule Mkuranga na Alpha Pharmaceuticals Ltd kilichopo Mbangala Rangi tatu, Temeke.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527