RAIS WA IRAN AZIHIMIZA NCHI ZA KIKANDA KUVIFUKUZA VIKOSI VYA MAREKANI

Rais Hassan Rouhani wa Iran amesema nchi za kanda ya Mashariki ya Kati zinapaswa kuvifukuza vikosi vya jeshi la Marekani kutoka kwenye kanda hiyo.

Rais huyo ameyasema hayo alipokutana na waziri mkuu wa Syria Bw. Imad Khamis ambaye yupo ziarani nchini Iran. 

Amesema nchi za kanda hiyo zinapaswa kujitahidi kumaliza uwepo wa vikosi vya Marekani, na kuwafukuza wakaliaji kutoka kanda hiyo.

Bw. Khamis amesema uwepo wa vikosi vya Marekani nchini Syria ni mfano mzuri wa ukaliaji, na nchi za kanda hiyo zinapaswa kujitokeza kupinga uwepo haramu wa vikosi vya Marekani katika kanda hiyo.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post