RAIA WATATU WA MAREKANI WAUAWA KENYA....PENTAGON YASEMA TUKIO HILO HALINA UHUSIANO NA MZOZO WA IRAN


Wafanyakazi watatu wa Wizara ya Ulinzi ya Marekani wameuawa kwenye shambulizi la kigaidi katika kambi ya kijeshi ya Manda ilioko mjini Lamu.


 Wafanyakazi 2 pamoja na makandarasi wawili wameripotiwa kuachwa na majeraha mabaya kufuatia shambulizi hilo la Jumapili, Januari 5. 

" Wakati wa shambulizi hilo la kigaidi katika kambi ya kijeshi ya Manda, wafanyakazi wa wizara ya ulinzi ya Marekani waliuawa, huku wengine wawili wakijeruhiwa vibaya ila hawako katika hali mbaya,"Sehemu ya taarifa ya ubalozi wa Marekani ilisoma. 

Aidha, Marekani imeapa kupambana vilivyo na magaidi wa al- Shabaab hasa wale waliotekeleza shambulizi la Manda. 
Hata hivyo, imesema tukio hilo halina uhusiano wowote na mzozo unaoendelea kati yake na Iran 


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527