NATO KUANGAZIA UPYA MPANGO WA MAJESHI YAKE IRAQ


MUUNGANO wa kujihami wa NATO unakutana leo kujadili mustakabali wa ujumbe wake wa kutoa mafunzo nchini Iraq wakati ambapo mivutano Mashariki ya Kati inaongezeka baada ya Marekani kumuua jenerali wa ngazi ya juu wa Iran.
 

Mabalozi kutoka nchi ishirini na tisa wanachama wa NATO wanatarajiwa kukutana katika makao makuu muungano huo mjini Brussels

Hali imezidi kuwa mbaya nchini Iraq ambapo wabunge wametaka kuondolewa kwa wanajeshi 5,200 wa Marekani walioko nchini humo


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527