MNYIKA KUGOMBEA TENA UBUNGE KIBAMBA


Katibu Mkuu wa Chadema, John Mnyika amesema atagombea tena ubunge Kibamba katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba, 2020.

Mnyika ambaye alichaguliwa kuwa katibu mkuu wa Chadema Desemba 20, 2019 ameeleza hayo leo Jumatano Januari 29, 2020 katika mahojiano maalum yaliyorusha moja kwa moja na Kituo cha Televisheni cha ITV.

Alipoulizwa kama atagombea tena ubunge katika jimbo hilo aliloliongoza tangu mwaka 2015,  Mnyika amewataka wananchi wajiandae kumchagua kuwa mwakilishi wao bungeni.

Amesema kwa kuwa wananchi walimchagua kuwa mbunge mwaka 2015 akiwa naibu katibu mkuu wa Chadema, pia watamchagua akiwa katibu mkuu wa chama hicho kikuu cha upinzani nchini.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527