MCHUNGAJI AMUUA MKEWE KANISANI KISA MCHEPUKO KANISANI


MCHUNGAJI mmoja nchini Kenya amemuua mkewe, Ann Mghoi,  kwa kumchoma visu, kisha na yeye kujiua.

Mchungaji huyo aliyefahamika kwa jina la Elisha Misiko alimuua mkewe ndani ya kanisa lake lililopo katika kijiji cha Chembani, Kisauni, Mombasa na baadaye kujikata koo hadi kufa.

Misiko aliyekuwa mchungaji wa kanisa la Goods for God’s Gospel Ministries ameacha ujumbe unaomlaumu mkewe kwa kuwa na mahusiano na kijana mdogo katika kanisa hilo, lakini pia katika ujumbe huo amemlaumu mkewe kwa kumzuia kuwaona watoto wao.

Mmoja wa polisi wa Kisauni, Julius Kiragu, ameeleza kuwa mchungaji huyo ameacha makaratasi 17 yaliyoandikwa kama wosia wake akibainisha sababu za kuchukua maamuzi hayo. 

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527