KAMWELWE: MUDA WA KUSAJILI LAINI ZA SIMU HAUTAONGEZWA


Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, Isack Kamwelwe amesema serikali haitaongeza muda wa kusajili laini za simu kwa alama za vidole, huku akitahadharisha kuwa katika siku zilizosalia, kasi ya wizi wa kimtandao kupitia simu za mkononi imeongezeka.

Amesema hayo jijini Dar es Salaam alipozungumza na waandishi wa habari kuhusu siku zilizobaki kabla ukomo wa siku 20 alizotoa Rais John Magufuli, haujawadia. Mwisho wa usajili ni Januari 20 mwaka huu.

“Kumejitokeza wizi wa kimtandao; wananchi tuwe macho sana tunapomalizia hizi siku zilizosalia kabla laini ambazo hazijasaliwa hazijazimwa. Watu wanatumia siku chache zilizosalia kuibia watu kwa kiwango cha juu; bila kuwa makini, watu tutaibiwa sana,” alihadharisha Waziri Kamwelwe.

Waandishi wa habari walipotaka kujua kama siku za usajili huo kwa alama za vidole zitaongezwa, waziri alisema: “Hakuna siku kuongezwa; siku za usajili hazitaongezwa.”


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post