ASTON VILLA YATANGAZA RASMI KUMSAJILI MBWANA SAMATTA


Klabu ya Aston Villa ya England, imetangaza kumsajili mshambuliaji wa kimataifa kutoka Tanzania Mbwana Samatta. 


Usajili wa Mbwana Samatta unatarajiwa kuimarisha safu ya mashambulizi ya timu ya Aston Villa ambayo imekuwa ikilegalega katika ligi ya Premier.

Aston Villa imecheza mechi zake tatu zilizopita bila mshambuliaji wa kutambuliwa baada ya mshambuliaji wao raia wa Brazil Wesley Moraes kujeruhiwa hivyo kutoweza kucheza tena msimu huu. 

Samatta aliyekuwa akiichezea klabu ya Genk nchini Ubelgiji, amefunga mabao kumi katika mechi zote likiwemo bao alofunga dhidi ya Liverpoool katika ligi ya Mabingwa uwanjani Anfield

Yeye ndiye mchezaji wa kwanza kutoka Tanzania kuwahi kusajiliwa na timu katika ligi ya Premier.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527