VIONGOZI 6 WA SERIKALI YA WANAFUNZI CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM WASIMAMISHWA MASOMO KWA MUDA USIOJULIKANA


Viongozi sita wa Serikali ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam – UDSM, (DARUSO), akiwemo Rais wao, Hamis Musa Hamis wamesimamishwa masomo kwa muda usiyojulikana kufuatia madai ya mikopo iliyochelewesha na Bodi ya Mikopo ya Wanafunzi wa Elimu ya Juu (HESLB) kwa wanafunzi wa chuo hicho.



Juzi, DARUSO ilitoa saa 72 kwa bodi ya mikopo ( HESLB) kutekeleza maagizo 4 likiwemo kuwawekea fedha za kujikimu wanafunzi ambao hawajapewa tangu Chuo kilipofunguliwa na Kama agizo hilo halitatekelezwa watakusanyika nje ya Ofisi hizo.

Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce Ndalichako, jana Jumanne, Desemba 17, 2019, aliupa uongozi wa chuo hicho saa 24 kuwachukulia hatua wanafunzi waliotoa tamko hilo na kusema  lilitolewa kinyume cha utaratibu na ni utovu wa nidhamu.

Viongozi wengine waliosimamishwa masomo kwa muda usiojulikana na uongozi wa chuo hicho ni Waziri wa Mikopo, Waziri wa Habari, Mwenyekiti wa Bunge na Jaji wa Mhimili isipokuwa Makamu wa Rais na inaelezwa kwamba wamepewa muda hasi saa 6 mchana wa leo wasionekane chuoni hapo.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527