UTURUKI KUTUMA VIKOSI VYA JESHI NCHINI LIBYA


Rais wa Uturuki Recep Tayyip Erdogan, amesema leo kuwa Uturuki itawatuma wanajeshi nchini Libya, kwa kuwa nchi hiyo ya kaskazini mwa Afrika imetoa ombi hilo. 

Erdogan amesema atawasilisha mswada kuhusu ombi hilo katika bunge la Uturuki mwezi Januari. 

Hapo jana, Rais Erdogan aliizuru Tunisia kujadiliana na mwenyeji wake Rais Kais Saied, kuhusu ushirikiano na uwezekano wa kusitisha machafuko nchini Libya. 

Kwenye hotuba yake leo, Erdogan amesema Tunisia ilikubali kuiunga mkono serikali ya Libya inayoungwa mkono na Umoja wa Mataifa na inayoongozwa na Fayez al-Serraj.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527