NDEGE YA TANZANIA ILIYOKAMATWA CANADA YAACHIWA....RAIS MAGUFULI KASEMA ITAPOKELEWA JIJINI MWANZA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt John Pombe Magufuli, amesema kuwa Ndege ya Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL) aina ya Bombadier Q400, iliyokuwa ikishikiliwa nchini Canada imekwishaachiwa huru.

Rais Magufuli ametoa taarifa hiyo leo Desemba 12, 2019, Jijini Mwanza, wakati akifungua semina ya Wajumbe wa Halmashauri Kuu Taifa (NEC) ya Chama cha Mapinduzi (CCM).

"Kwanza kwa taarifa tu Ndege yetu iliyokuwa imeshikwa Canada imeachiwa, mtatangaziwa tarehe ya kuipokea na mtaipokea hapa hapa Mwanza" amesema Rais Magufuli.

Taarifa za kukamatwa kwa Ndege hiyo zilitolewa siku ya Novemba 23, 2019, Ikulu ya Chamwino, Jijini Dodoma na Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Profesa Palamagamba Kabudi.


==>>Msikilize hapo chini


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527