Picha : CHIPUKIZI WA UMOJA WA VIJANA CCM TAIFA WAKUTANA DODOMA KUCHAGUA VIONGOZI WAO WA KITAIFA



Meza Kuu Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana Mwl Raymond Mwangwal (katikati) kulia ni Mwenyekiti wa Chipukizi Taifa anayemaliza muda wakeNdg Nimka Stanley pamoja na Makamu mwenyekiti wa Chipukizi Taifa anayemaliza Muda wake Ndg Pili Suluhu Hassan. Mkutano Mkuu wa saba wa Chipukizi Taifa unafanyika katika Ukumbi wa Sekondari ya Dodoma leo tarehe 14/12/2019 jijini Dodoma.
Meza Kuu
Chipukizi Wakifurahi
Kaimu Katibu wa Idara ya Uhamasishaji na Chipukizi Ndg Leonard Singo akitoa maelezo
Chipukizi akifurahi 
Mwenyekiti wa Chipukizi Taifa anayemaliza muda wake Ndugu Nimka Stanley Lameck akiongea na wajumbe wa Mkutano Mkuu wa saba wa Chipukizi Taifa unaofanyika katika Ukumbi wa Sekondari ya Dodoma leo tarehe 14/12/2019 jijini Dodoma.
Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa saba wa Chipukizi Taifa wa Umoja wa Vijana wa CCM wakimsikiliza kwa makini Mwenyekiti wa Chipukizi Taifa anayemaliza muda wake Ndugu Nimka Lameck katika Mkutano Mkuu wa saba unaofanyika jijini Dodoma.
Makamu Mwenyekiti wa Chipukizi wa Umoja wa Vijana Taifa Ndugu Pili Suluhu Hassani akiaga wajumbe wa Mkutano Mkuu wa saba wa Chipukizi Taifa unaofanyika jijini Dodoma.
Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa saba wa Chipukizi Taifa wakiwa katika shamrashamra za Uchaguzi wa kuchagua Viongozi wapya wa Chipukizi Taifa.
Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi Ndugu Raymond Mwangwala akitoa Hotuba katika Mkutano Mkuu wa saba wa Chipukizi wa Umoja wa Vijana wa CCM Taifa unaofanyika jijini Dodoma.
Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chipukizi Taifa wakisikiliza kwa makini hotuba ya Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa CCM Taifa Ndugu Mwl Raymond Mwangwala.
Wajumbe wa Mkutano Mkuu wa Chipukizi Taifa wakiwa tayari kwa Uchaguzi Viongozi wapya wa Chipukizi Taifa katika Mkutano Mkuu wa Chipukizi Taifa unaofanyika jijini Dodoma.

Katibu Mkuu wa Umoja wa Vijana wa Vijana Wa Chama Cha Mapinduzi (Katikati)Mwl Raymond Mwangwala akivikwa Skafu na Chipukizi wa Umoja wa Vijana alipowasili katika Ukumbi wa Shule ya Sekondari Dodoma Unapofanyika Mkutano Mkuu wa Chipukizi Taifa

Picha zote na Fahadi Siraji wa UVCCM

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527