PROF. KUFUNGUA MKUTANO WA WATAFITI 250 WA SAYANSI KUTOKA NCHI MBALIMBALI


Kushoto ni Meneja tafiti Costech,katikati ni Mkurugenzi mkuu Costech Dr Amos Ningu na Afisa Mtafiti kutokaTume ya Sayansi na Teknolojia NeemaTindamalile (kulia).


Na Hellen Kwavava Dar es Salaam

Waziri wa Elimu,Sayansi naTeknolojiaProfesa Joyce Ndalichako leo jioni anatarajia Kufungua Mkutano Mkuu wa mwaka wa baraza la sayansi kanda ya Afrika utakaofanyika hotel ya Sea Clif jijini Dar es Salaam.

Mkutano huo unaohusisha wanasayansi 250 toka nchi mbalimbali na Tanzania ikiwani Mwenyeji wake.

Akizungumzia kuhusiana na mkutano huo Afisa Mtafiti kutokaTume ya Sayansi na Teknolojia NeemaTindamalile alisema mkutano utafanyika wiki nzima na mada mbalimbali zitajadiliwa kila siku ilikuongezeana uelewa katika sayansi uwazi

“Mkutano huu unatarajia kuanza leo Jumatatu Novemba 11,2019 na kuna mada mbalimbali zitajadiliwa ambapo siku ya kesho kutakuwa na mada ya sayansi uwazi katika utafiti na ubunifu kwa ajili ya maendeleo lakini pia kutajadiliwa mada ya Jinsia mbalimbali katika ubunifu”,alisema Neema.

Naye Hulda Gideon alisema lengo la Mkutano huo nikufanya sayansi zote zijumuishe watu alafu ziwe na uwazi iliziweze kuwafikia walengwa kwa ufasaha.

“Tunaposema sayansi uwazi inahusisha mambo tofauti tofauti katika kufanya tafiti kwa uwazi zaidi ambapo inaanzia katika wazo kwa kuliweka wazi,Vifaa vya Utafiti kuwa wazi ili watu wengine wajue pia nanamna ya kufundisha masuala ya Utafiti kwa Uwazi”,alisema Hulda.

Hata hivyo Mkurugenzi Mkuu wa Costech Dr Amos Ningu aliongeza kwamba kwenye Mkutano huo utaleta ushirikiano zaidi kati ya taasisi mbalimbali toka nje kwa kuboresha kazi baina yao watafiti na kuzifanya ziwe za kiwango cha juu zaidi.

Mkutano huo umeweza kughalimu kiasi cha shiling Milion mia tano na wanasayansi hao wataweza kutembelea vivutio mbalimbali vya utalii nchini.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527