
Profesa Lipumba ametoa msimamo huo leo Jumanne Novemba 12, 2019 wakati akitoa maazimio ya kikao cha baraza kuu la uongozi la CUF.
CUF kinakuwa chama cha siasa cha sita kujitoa katika uchaguzi huo baada ya Chadema, ACT-Wazalendo, NCCR-Mageuzi, UPDP na Chauma.
Katika maelezo yake Profesa Lipumba amesema baraza hilo limetafakari kwa kina na kuona hakuna umuhimu kushiriki uchaguzi baada ya hoja zao tatu walizoziwasilisha serikalini kutofanyiwa kazi.
Profesa Lipumba amewataka asilimia nne ya wagombea wa chama hicho waliopitishwa kugombea kujitoa na kuiomba Tamisemi kutotumia nembo ya chama hicho kwenye uchaguzi huo.
Social Plugin