UCHAGUZI MKUU CHADEMA KUFANYIKA DESEMBA 18, 2019

Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema kimetangaza ratiba ya uchaguzi wa viongozi wake ngazi ya Taifa.


Mchakato huo unaanza na uchukuaji na urejeshaji fomu kuanzia  Novemba 18 hadi Novemba 30, 2019 huku mkutano mkuu ukifanyika Desemba 18, 2019.

Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Vicent Mashinji akizungumza na wanahabari makao makuu ya chama hicho, Kinondoni jijini Dar es Salaam alisema uchaguzi huo utaanza kwa kuchagua viongozi ngazi ya mabaraza na kufuatiwa na viongozi wakuu wa chama ngazi ya Taifa.


"Tutakuwa na Mkutano Mkuu wa Taifa itakuwa December 18, 2019, tushapeleka mialiko kwa watu mbalimbali, miongoni mwa mambo tutakayoyafanya siku hiyo ni kuchagua Viongozi Wakuu wa Chama

"Mchakato tunaoanza nao ni kuchukua na kurudisha fomu za Wagombea, huu mchakato unaanza November 18, 2019, wote ambao wangependa kugombea nafasi mbalimbali wanakaribishwa kuja kuchukua fomu, kujaza kwa ufasaha na kwenda kugombea" Amesema  Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Vicent Mashinji

Amesema baada ya kupitia majina ya wote walioomba, Desemba 8, 2019 kamati tendaji ya baraza la vijana na wazee watakutana na kufuatiwa na mkutano mkuu wa uchaguzi wa viongozi wa mabaraza hayo Desemba 9, 2019.

Dk Mashinji amesema Desemba 10, 2019 kamati tendaji ya baraza la wazee na vijana itakutana ambapo ni vikao vinavyofanyika kufuatiwa na mkutano mkuu.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527