TAKUKURU YAMKAMATA MWEKA HAZINA WA KIKUNDI ALIYEDAI PESA ZIMEYEYUKA KISHIRIKINA

Taasisi ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa (TAKUKURU) Mkoa wa Arusha inamshikilia Muweka hazina wa kikundi cha ujasiriamali cha Imani kwa tuhuma za kutafuna Tsh.Million 39 za Wanakikundi na kudai zimeyeyuka kishirikina.


Wanakikundi 28 juzi walikesha wakilia nyumbami kwa Muweka hazina huyo Halima Mwidadi Mkazi wa Osunyai Arusha baada ya kuambiwa fedha hizo ambazo walitakiwa kugawana zimepotea katika mazingira ya kutatanisha.

Wengine waliokamatwa na TAKUKURU ni Katibu wa Kikundi Deogratius Seif na Mwenyekiti wake Aisha Saidi ambao walikamatwa jana na kuachiwa kwa dhamana huku Muweka hazina akiendelea kusota Mahabusu kwa sababu za kiupelelezi.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527