SIMBA SC YAMTIMUA KOCHA PATRICK AUSSEMS


Aliyekuwa kocha wa Simba Patrick Aussems
Kocha wa Simba Patrick Aussems amesema uongozi wa Simba umemthibtitishia kuwa yeye kuanzia sasa si Kocha tena wa Klabu hiyo.

Aussems amesema hayo kupitia ukurasa wake wa Twitter ambapo amesema uongozi wa Simba na kupitia Mkurugenzi wake ndiyo umempatia taarifa hizo.

Aussems ameandika kuwa "Kupitia Bodi ya Wakurugenzi wa Simba nimeambiwa mimi si Kocha tena wa timu hiyo."

Hivi karibuni timu hiyo ilitangaza kumsimamisha kazi Kocha huyo kwa kile ilichoelezwa ni utovu wa nudhamu

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527