RC MONGELLA AZINDUA MAADHIMISHO YA MAULID KITAIFA JIJINI MWANZA

Mkuu wa Mkoa
Mwanza, John Mongella (katikati) amezindua rasmi wiki ya maadhimisho ya sikukuu ya Maulid
inayofanyika kitaifa jijini Mwanza. 
Uzinduzi huo
ulifanyika Novemba 04, 2019 katika uwanja wa Furahisha ambapo Sikukuu ya
Maulidi inatarajiwa kufanyika Novemba 09, 2019.



Sikukuu ya Maulid mara ya mwisho ilifanyika mkoani Mwanza zaidi ya miaka 20 iliyopita hivyo kufanyika mwaka huu 2019 (1441) ni neema kubwa huku jambo jema zaidi likiwa ni ushirikiano baina ya dini zote.
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella akionesha kanga zenye ujumbe wa Maulid 2019 kama ishara ya uzinduzi wa sikukuu hiyo.
Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella akizungumza kwenye hafla ya uzinduzi wa Maulid.
Sheikh Issa Othuman Issa kutoka Baraza la U'lamaa BAKWATA akitoa salamu zake kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi kuzindua Maulid 2019.
Sheikh wa Mkoa Mwanza, Sheikh Hassan Kabeke akitoa salamu zake kwenye hafla hiyo.
Viongozi mbalimbali wakiwa kwenye uzinduzi wa Maulid kitaifa jijini Mwanza.
Mkuu wa Mkoa Mwanza (wa pili kushoto) akipata maelezo baada ya kutembelea banda la Shirika la kutetea haki za wasichana na wanawake KIVULINI ambalo ni miongoni mwa wadau walioshiriki maonesho ya wiki ya Maulid 2019.
Tazama Video hapa chini





Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527