RAIS MAGUFULI APIGA SIMU LIVE KONGAMANO LA SANAA LA MWALIMU NYERERE LIKIENDELEA


Rais Magufuli amempigia simu rais wa Chama cha Muziki wa Injili Tanzania, Ado Novemba na kumwambia anafuatilia shughuli hiyo ya kongamano la Sanaa la Mwalimu Nyerere.

Kongamano la Sanaa la Mwalimu Nyerere linafanyika katika Ukumbi wa Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC) Jijini Dar es salaaam.

"Nakusikiliza usiwe na wasiwasi na maagizo yangu niliyoyatoa Waziri Mkuu atayawasilisha hapo kwenu, ninawapenda sana, wasanii oyeeee," alisema Rais Magufuli.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kassim Majaliwa anamuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. John Pombe Magufuli katika Kongamano hilo.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527