NAIBU WAZIRI WA AFYA AFUNGUA WARSHA YA WADAU WA UTAFITI KANDA YA ZIWA

 Naibu Waziri
wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile
akifungua warsha ya siku mbili kwa wadau wa utafiti/ watoa huduma za afya Kanda ya Ziwa.


Warsha hiyo yenye lengo la kuwajengea uwezo watoa huduma za afya wakiwemo Waganga Wakuu wa Mikoa na Wilaya kushirikiriki katika tafiti imefanyika Novemba 04, 2019 jijini Mwanza ikiandaliwa na Taasisi ya Taifa ya
Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR).
Na George Binagi-GB Pazzo, BMG
 Mwenyekiti wa Baraza la NIMR, Dkt. Deodatus Mtasiwa akitoa salamu zake kwenye ufunguzi wa warsha hiyo.
 Mkurugenzi Mkuu NIMR, Prof. Yunus Mgaya akizungumza wakati wa warsha hiyo.
 Mkurugenzi wa Utafiti NIMR, Dkt. Paul Kazyoba akitoa ufafanuzi kuhusiana na warsha hiyo iliyowashirika watoa huduma mbalimbali wa afya wakiwemo Waganga Wakuu wa Mikoa na Wilaya Kanda ya Ziwa.
 Mkurugenzi wa NIMR Kituo cha Mwanza, Dkr. Safari Kanung'hi akitoa salamu zake kwenye warsha hiyo.
 Mkuu wa Wilaya Nyamagana, Dkt Philis Nyimbi akitoa salamu za Mkuu wa Mkoa Mwanza, John Mongella.
 Mgeni rasmi, Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dkt. Faustine Ndugulile (wa tano waliokaa) akiwa kwenye picha ya pamoja na viongozi na washiriki mbalimbali wa warsha hiyo.
Tazama Video hapa chini

NIMR yawapiga msasa watoa huduma za afya Kanda ya Ziwa






Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527