JESHI LA POLISI LAMSHIKILIA HALIMA MDEE....KUFIKISHWA MAHAKAMANI JUMATATU


Mbunge wa Kawe Halima Mdee anashikiliwa na Polisi katika kituo cha Oysterbay, kufuatia agizo la Mahakama ya Kisutu la kukamatwa kwa wabunge wanne wa CHADEMA.


Jeshi la Polisi Kinondoni limesema Mdee ameripoti mwenyewe kituoni hapo leo Novemba 16, 2019 na atafikishwa mahakamani siku ya Jumatatu.

'Ni kweli yupo hapa kituoni tunamshikilia kama ambavyo Mahakama iliagiza na yeye amekuja mwenyewe kuripoti hapa, hivyo taratibu zote za kipolisi zinafanyika na Jumatatu atafikishwa mahakami', amesema Msaidizi wa RPC Kinondoni.

Amri hiyo ya kukamatwa kwa wabunge hao Halima Mdee, Peter Msigwa, John Heche na Ester Bulaya, ilitolewa jana, Novemba 15, 2019 na Hakimu Mkazi Mkuu wa Mahakama hiyo Thomas Simba, ambapo alisema kuwa kesi hiyo ilifikishwa mahakamani hapo kwa ajili ya upande wa mashtaka kumhoji Mbowe na baada ya kumaliza kutoa ushahidi wake kutoka upande wa utetezi na ndipo ilipobainika washtakiwa hao wanne kutokuwepo mahakamani.
 


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527