FAMILIA YA MAREHEMU DAUDI BALALI YAMUOMBA RAIS MAGUFULI AWASAIDIE KUREJESHA MALI ZAO


Familia ya Marehemu Daudi Balali imemuomba Rais Magufuli kuisaidia kuokoa mali za Gavana huyo wa zamani wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT) ambazo inadai zimechukuliwa na Wajanja wa Mjini.

Balali aliyeripotowa kufariki Dunia Marekani Mei 16, 2008 alikuwa Gavana wa BOT katika Utawala wa Serikali ya Awamu ya Tatu chini ya Rais Mkapa.

Wakizungumza na Wanahabari Boko nje kidogo ya Dar, baadhi ya Ndugu wa Balali wakiwamo Kaka na Dada zake wamedai kupokwa mali za Ndugu yao kulianza 2012 baada ya watu wasiojulikana kuvamia kwa Mama yake (Rahel Balali) Boko na kuiba sanduku lililokuwa na nyaraka mbalimbali za marehemu ikiweno hati za mashamba, nyumba na viwanja.

"Tunaomba Rais atusaidie kuna mambo yanakwamishwa na baadhi ya Watumishi wa Serikali, tunapoona watu wa nje wanafanya uamuzi wa kubeba kila kitu tunaadhirika, tunateseka"


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527