CAG KICHERE ATAMBULISHWA BUNGENI


Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Charles Kichere leo Jumatatu Novemba 11, 2019 ametambulishwa rasmi bungeni jijini Dodoma, ambapo Spika Job Ndugai ameahidi kuwa, bunge litampatia ushirikiano mkubwa. 


"Nataka nimuhakikishie kuwa, Bunge litakupa ushirikiano wa kila aina na wala hatuna tatizo na ofisi ya CAG kwa hiyo tutakuwa pamoja," amesema Ndugai.

Spika amesema leo mchana atakutana na CAG na wenyeviti wa kamati pamoja ili wajadiliane pamoja na kuzungumza baadhi ya mambo.


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527